SAME YATAKA KUIMARISHA LISHE.

Kamati ya Lishe yazinduliwa Wilayani Same. Yahimizwa kuhakikisha Inapunguza kiasi cha udumavu Kutoka 29% ya sasa, ambayo Ndiyo ya Mkoa mzima wa Kilimanjaro.
Tanzania ya viwanda Na ya uchumi wa kati inataka watu wenye Lishe bora watakao kuwa Na akili nyingi, wabunifu Na wenye vipaji vya kufanya mambo makubwa. Yote hayo yanachangiwa Na Lishe bora. 
Alisema DC wa Same Mh. Rosemary Senyamule aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo Uliofanyika Tar. 07/09/2018.

Aliyesima ni Mh. Mkuu wa Wilaya ya Same na Upande wa  Kushoto ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Same Dr. Andrew na Upande wa kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndugu AnnaCaire Shija.